Wednesday, August 12, 2015

kennytz na Kenneth Paul

Blogu ya kennytz inayomilikiwa na Kenneth Paul ni blogu ya Kitanzania yenye dhumuni la kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili. Katika kennytz, utapata kusoma masimulizi mbalimbali yanayoandikwa na Kenneth Paul ambaye ni msomi mwenye upeo mkubwa wa kuelewa lugha. Masimulizi ya Kenneth Paul utakayoyasoma katika kennytz yatakuwa yakitumia lugha ya Kiswahili yenye usanifu mkubwa ili kupitia masimulizi hayo, uweze kupata picha yaani ufahamu juu ya matumizi sahihi ya lugha yetu ya Kiswahili. Hata hivyo baadhi ya masimulizi yanaweza kuwa katika lugha ya Kiingereza kwa ajili ya kutoa burudani kwa wale wapenzi wasiofahamu lugha ya Kiswahili.
Pia katika kennytz, kuna kipengele cha kucheka na kuchekesha ambapo kurasa zake zinalenga maswala ya vichekesho. Kenneth Paul ni kati ya watu wenye uwezo mkubwa wa kuchekesha na kupitia utaalamu wa Kenneth Paul wa kudadisi na kupembua mambo, amejaribu kutafuta mambo mbali mbali yanayohusiana na swala la kucheka na kuchekesha watu.
Kennytz itakupa mafunzo ya lugha ya maneno, yaani kusikiliza kwa umakini maneno watumiayo watu ili kuelewa dhamira ya mazungumzo. Vile vile katika kujifunza huko, utaweza kujua maneno sahihi ya kutumia ili kuweza kufanikisha malengo ya kauli zako, kama ni kuchekesha, kuuliza swali, kutoa taarifa, kuomba msamaha, kushawishi na mengine mengi.
Kennytz pia inajaribu kuelezea mafunzo mbali mbali kutoka katika filamu ndani na nje ya Tanzania. Kenneth Paul ni mpenzi wa filamu na amekuwa akijifunza mengi kuhusu maisha kupitia filamu. Lakini Kenneth Paul amekuwa akishangazwa na namna watu wanavyochukulia kwamba filamu zipo tu kwa ajili yta kuburudisha na si kufundisha. Hivyo Kenneth Paul anafichua mafunzo mbali mbali kutoka katika filamu kupitia kennytz ambayo yatasaidia watu katika maisha.
Karibu na tembelea kennytz ya Kenneth Paul mara kwa mara kwa ajili ya burudani na mafunzo.

No comments:

Post a Comment

  • Hadithi na Simulizi