Sunday, September 13, 2015

Roho ya Kayumbas: Sehemu ya 6




Kabla ya kukicha, majira ya saa kumi na moja na nusu alfajiri, baba Kayumbas anaamka na kuondoka kwenda kazini. Mama Kayumbas na akina Kayumbas wanaamka saa kumi na mbili na kufanya shughuli zao. Ndiyo ratiba yao ya siku zote.
Miezi kadhaa inapita huku maisha yakienda vizuri hata baba Kayumbas kuweza kuwanunulia wanawe runinga mwezi mmoja tu tangu akubaliane na mkewe swala hilo na sasa ameanza kuweka akiba kwa ajili ya  kununua kiwanja hapa Dar na baadaye kuweza kujenga nyumba ndogo kwa ajili ya familia yake.
Miezi inakwenda huku kila leo ikiwa kama jana na kesho kutegemewa kuwa kama leo hadi unapofika mwezi wa kwanza ambapo watoto wanapanda darasa moja mbele na Mjanja kuanza chekechea.

[Endelea kufuatilia simulizi hili litokanalo na matukio ya kweli...]

No comments:

Post a Comment

  • Hadithi na Simulizi